Tunapenda kumshukuru Mungu kwa kutulinda sote kipindi chote cha likizo na sasa tunaanza mwaka mpya wa masomo. Jina la Bwana Yesu libarikiwe. Taarifa ni kama ifuatavyo:

i.Tutaanza na ratiba za ibada za katikati ya week kwanzia tarehe 2/11/2015 siku ya Jumatatu, Jumatano, Ijumaa kwanzia Saa kumi Jioni. Pale Ukumbi wa M-4 na Jumapili tarehe 08/11/2015 tutakuwa na Ibada ya Jumapili katika ukumbi wa M-11.

ii.Tunapenda kuwakumbusha wana USCF wote kujisajili njia ya mtandao kupitia www.uscfsaut.blogspot.com   usajili umeanza kuanzia leo tarehe 29 October.

iii. Tunawaomba wote kama kuna mtu  ana ndugu/rafiki ambaye ni first year na amepangwa SAUT -Mwanza aweze kutupa mawasiliano yake ili Uongozi wa USCF uweze kumpokea na kumwandalia mazingira mazuri ya kuishi chuoni. Pia mkaribishe ajisajili kupitia www.uscfsaut.blogspot.com

   Kama una lolote unaweza kuwasiliana nasi.